WIZARA YA MADINI YASAINI MKATABA UJENZI WA MAJENGO PACHA YA GHOROFA 8 YA KITUO CHA TGC
Wizara ya Madini imesaini Mkataba wa Ujenzi wa Jengo la kisasa la ghorofa nane la Kituo cha Jemolijia Tanzania (TGC) na Kampuni mbili za wazawa zilizoungana za Skywards na Lumocons.
Hafla hiyo imefanyika leo Juni 26, 2024 katika Ukumbi wa Mikutano wa Prof. AbdulKarim Mruma jijini Dodoma na kushuhudiwa na Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa.
Kwa upande wa Wizara, Mkataba ho umesainiwa na Katibu Mkuu Kheri Mahimbali huku Mkurugenzi wa Kampuni Lumocons Limited Innocent Shirima akisaini kwa niaba ya Kampuni hizo mbili za ujenzi.
Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Kiruswa amewataka wazabuni hao kuhakikisha wanakamilisha ujenzi wa jengo hilo kwa ubora na muda unaotakiwa na kwamba Wizara ya Madini itatoa ushirikiano ili kuhakikisha kutokuwepo kwa vikwazo vyovyote muda wote wa ujenzi.
Ujenzi wa Jengo hilo la TGC utagharimu kasi cha shilingi bilioni 33.42 (33,429,365,267.00) mpaka kukamilika.